This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday 23 July 2015

TARIBO WEST AKIRI ALIKUA ANATUMIA UCHAWI KUCHEZA SOKA

Mlinzi wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria maarufu kama Supper Eagles, hivi karibuni alitoa ushuhuda wa ajabu na kuwashtua watu wengi.
Taribo West ambaye alikuwa ni kivutio sana uwanjani enzi za ujana wake akiwa na Supper Eagles sasa ameokoka na kuwa mchungaji.
Taribo alishuhudia kwamba alikuwa akipelekwa na meneja wake nchini Senegal kwa waganga wa kienyeji ili aupige mwingi uwanjani.
Taribo West anasema alikatwa baadhi ya sehemu za ulimi, vidole na kisha kupikwa jikoni pamoja na mambo mengine ili acheze vizuri akiwa uwanjani.
Beki huyo wa zamani wa kutumainiwa wa Nigeria ambaye amekuwa ‘Pastor’ hivi sasa anasema alitembelewa na mwanamke wa Mungu, ajulikanaye kama sister Ikemefunwa akiwa nchini Italia, na kisha kumuombea na kuutoa uchawi wote na kumuweka mtu safi.
Baada ya kumaliza soka, Taribo West sasa anamtumikia Mungu kwa kutangaza maneno yake.

Tuesday 14 July 2015

MZEE YUSUPH AMESEMA INABID AACHE MZIKI KABISA

Lazima niache muziki- Mzee Yusup Mwimbaji mahiri wa muziki wa Taarab nchini ambaye pia ni mkurugenzi wa kundi la Jahazi Modern Taarabu, Mzee Yusuph amefunguka na kusema kuwa lazima aache muziki na kufanya kazi zingine nje ya muziki

Mzee Yusuph alisema hayo alipohojiwa na mtangazaji wa Tam Tam za Mwambao ya East Africa Radio, Mwanne Othman.
Mzee Yusuph alisema kuwa kwa sasa anataraji kutoa album mbili za mwisho ili aweze kuachana na muzuki kwa swababu ana mambo mengi ya kufanya hasa siasa na kazi zake na badala yake atakuwa boss tu kwa wasanii wenzake katika kundi lake hilo ila si uimbaji tena.
"Muda ikifika nitaacha, lazima niache muziki kwa sababu nina mambo mengi ya kufanya nje ya muziki, na kama hivyo nikipita katika nafasi ya ubunge itabidi tu nicahgue moja itabidi kwenye muziki nisipatikane kwa asilimia mia moja vivyo wapenzi wa muziki wangu lazima waelewe kuwa naacha muziki kwa sababu ya siasa na kazi zangu zingine ambazo ni nyingi na zinahitaji uwepo wangu hivyo lazima niache muziki ili niweze kukamilisha mambo mengine nikiwa nje ya muziki."
Lakini mzee Yusuph aliweza kuweka wazi suala la yeye kutaka kugombea nafasi ya ubunge katika jimbo la Fuweni Zanzibar na kusema kuwa anataka kulipa fadhila kwa namna ambavyo mashabiki wake walivyoweza kumpenda na kumjali na kuweza kumfanikishia mambo mengi kupitia njia ya muziki, hivyo yeye anaamini ubunge ni wito anaona bora awe mbunge ili jamii iweze kumtuma na kuwawakilisha wananchi katika mambo yao kwa kuwa wananch9o hao wameweza kumletea mabadiliko katika maisha yake ya kawaida.
Mbali na hilo Mzee Yusuph ameeleza kuwa yeye kuingia katika siasa si lengo ya kutafuta kutoka kimaisha bali anaamini anaweza kuwafanya jambo wananchi kwa kujitolea maana lengo lake ni kuwatumikia wananchi.
"Mimi sina ndugu sina baba ambaye ni kiongozi bali nimeingia katika siasa ili wananchi waweze kunituma maana mimi naamini hii kazi ni ya wito tu hivyo wananchi wasiangalie majina ya viongozi bali waangalie mtu mwenye dhamira njema ya kutaka kufanya jambo kwa manufaa ya wananchi na kwa kujitolea. Mimi naanzia kwenye ubunge ikiwezekana huko baadaye mpaka kwenye urais nitafika tu"

DILI LA STERLING KWENDA MANCHESTER CITY LIMETICK

Sakata hili lililoteka hisia za mashabiki duniani kote ikiwa ni pamoja na vyombo vya habari, limefikia tamati wakati ambao timu zinajiandaa na msimu mpya. Juzi Raheem Sterling alitajwa kwenye kikosi kitakacho safiri na kikosi cha Liverpool kuelekea kwenye mechi za pre-season, jana zikatoka habari kwamba hatasafiri na kikosi hicho.
Leo hii hatimaye klabu za Liverpool na Manchester City zimefikia makubaliano katika sakata la usajili wa kiungo mshambuliaji wa Liverpool, Raheem Sterling na kutua City kwa ada ya uhamisho wa pauni 49m.
Katika makubaliano baina ya vilabu hivyo vya uingereza, Manchester City watalipa pauni 45m kwanza na kisha kuongeza pauni 4m kutokana na ushiriki wa Raheem katika kikosi hicho za Manchester.
Liverpool walikataa ofa ya kumuuza mchezaji huyu kwenda City zaidi ya mara mbili huku wakikomaa kupata pauni 50m kwa kijana huyu mwingereza mwenye asili ya Jamaica.
Sterling ambae majuma kadhaa yaliyopita alitajwa kama mmoja wa wanandinga wenye thamani zaidi chipukizi, amewachukiza sana mashabiki wa Liverpool ambao wanamuona dogo huyo kuwa mkosa adabu na heshima kwa klabu.
Aidha nahodha aliyeondoka kikosini hapo dirisha hili, Steven Gerrard amekaririwa akimlaumu mchezaji huyo kwa kukosa subira ya mafanikio ndani ya Liverpool na kuhofia kwamba litakua si jambo jema kwa Raheem kukaa benchi Manchester City wakati anapata nafasi kikosi cha kwanza, akiwa na Liverpool

HAYA SASA KWA WALE WA CHELSEA , MOURINHO ANATAKA SAINI YA HUYU NYOTA WA BARCELONA

Mwanzoni kabisa wa kipindi cha usajili Jose Mourinho alisema kwamba kwenye kipindi hiki cha usajili hatafanya sana usajili kwasababu anakikosi kizuri. Lakini pia alisema atafanya usajili mdogo tu kuziba sehemu ambazo anadhani zinahitaji usajili.
Kocha Jose Mourinho wa Chelsea amepanga kuwania saini ya mshambuliaji Mhispania, Pedro Rodriguez anayekipiga Fc Barcelona kwa ada ya pauni milioni 22.
Pedro ambaye hafurahii maisha hivi sasa kutokana na kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza cha mabingwa hao wa Ulaya. Mfumo wa sasa wa 4; 3; 3 unamnyima nafasi Pedro kutokana na uwepo wa Messi, Suarez na Neymar.
Gazeti la Sports la nchini Uhispania linaripoti kuwa kijana huyo hatakiwi katika kikosi hicho na hivyo anaweza kuondoka katika majira haya ya joto.

Inaelezwa kuwa Barcelona wako tayari kumuachia mshambuliaji huyo kwa ada ya pauni 22m.
Pedro ambaye hapati nafasi hivi sasa katika kikosi cha Barcelona anaamini anaweza kupata dakika nyingi za kucheza tofauti na ilivyo sasa Camp Nou.
Kuelewana kwa ushirikiano wa washambuliaji watatu wa kiwango cha dunia, Messi, Suarez na Neymah unamfanya kocha wa Barcelona, Luiz Enrique kutomuangalia Pedro.

wazazi wa Iker Cassilas wamchana Florentino Perez ....

Wazazi wa Iker Casillas wamesema kuwa, kuondoka kwa mtoto wao katika klabu yake pendwa ya Real Madrid ni kutokana na kampeni chafu inayoendelea kutoka kwa rais wa klabu hiyo Florentino na kusisitiza kuwa, mtoto wao alipaswa kumalizia maisha yake ya soka katika klabu yenye hadhi ya juu na si kama klabu aina na Porto.
“Mbona wakati wa marais Lorenzo Sanz na Ramon Calderon, alikuwa akilelewa vema,” waliiambia El Mundo.
“Lakini Florentino Perez kamwe hakumpenda. Rais huyu kamwe hajawahi kumpenda, sababu kubwa ni kutokana na ufupi wake”.
“Iker amekumbana na mambo mengi ambayo hayajawahi kuandikwa. amepata matatizo makubwa ya kisaikolojia na amekuwa akichukuliwa tofauti na wachezaji wengine. Amekuwa ni kiungo muhimu sana ndani ya miaka mitano iliyopita lakini imekuwa ni suala tofauti kabisa na wanavyomfanyia hapa.”
Mama yake, Maria del Carmen Fernandez, aliongeza: “Florentino Perez ndio chanzo kikubwa sana kwa Iker kuondoka hapa Madrid. Ndio, ni kweli mwanangu amekuwa akipata ofa nyingi sana, lakini Florentino hakutaka yeye aende kwenye vilabu vikubwa. Hataki mwanangu afanikiwe.
“Porto ni timu ambayo iko katika levo sawa na timu ya daraja la pili ya Segunda B, mwanangu anahitaji timu iliyo juu zaidi ya hapo kama Barcelona.
“Kipa bora wa dunia hawezi kumalizia maisha yake ya soka katika klabu  kama ya Porto! Nisingekasirika kama mwanagu angeenda Barcelona kwa sababu ni timu bora.”
Jose Luis Casillas anahisi kuwa sehemu kubwa ya vyombo vya habari vilikuwa vikimsapoti Perez kumuandama mlinda mlango huyo mkongwe.
“Kampeni hii chafu ilinza kuundwa na Florentino huku akipewa sapoti na na baadhi ya waandishi na vyombo vya habari tangu mwaka 2010.”

50 cent hatarini kufilisika

Moja ya wasani maarufu duniani na nyota wa miondoko ya hiphop, rapa 50 Cent , aomba sheria ya kufilisika yenye kifungu cha 11 imlinde na mali zake huko marekani.
Hoja hiyo ilikuja siku chache baada ya mahakama kuamuru rapa huyo alipe dola za kimarekani milioni tano kwa mwanamke aliemshitaki kwakile alichokisema kuwa aliweka video chafu mitandanoni bila ya ridha yake.
Mwanamziki huyo mwenye jina halisi la Curtis James Jackson wa tatu ameuza zaidi ya albamu milioni thelathini duniani kote

Team ya manchester united ikiwa taari kwa safari kuelekea marekani kwa maandalizi ya msimu ujao......

Friday 27 March 2015

Rooney : sitashangilia tena kwa mtindo wa boxing

Wayne Rooney amesema kwamba hatoshangilia tena kwa mtindo wa 'boxing' kwa sababu mkewe alimuona mwanae wa kwanza Kai akiiga ushangiliaji wa baba yake darasani akiigiza kupigana na wenzie.

HUYU NDIO MBUNGE MZURI ZAIDI TANZANIA...... BONGO MOVIES WOTE WANAKAA CHINI ANIII...... jina lake Catherine Magige





Catherine Magige Mbuge wa Arusha atajwa kua mbunge mzuri zaidi,, ana mvuto wa sura,, shape analo yuko vizuri aseeeeee!!!!! Ukimuangalia fasta fasta bila kuambiwa anafanya kazi gani,, utasema anacheza sinema za Bongo movies lakini lahashaa. Yeye ni mbunge mwenye mvuto wa aina yake... yuko smart, photogenic, na sifa nyingine nzuri ni nouma sanaaaaaa 

Agness Masogange atwajwa kua mwanamke mzuri zaidi TANZANIA

Huyu ni mwanamke mzuri Tanzania kutokana na jarida moja la Nigeria. Anaitwa Agness Masogange. Kwa sasa anakula bata huko bondeni kwa Madiba..... wewe una maoni gani? je ni kwel ndo mwanamke mzuri Tanzania?

Friday 20 February 2015

Huyu ndiye mkuu mpya wa wilaya ya Iramba mh. LUCY MAYEMBA aliyeteuliwa na J.K. Sema neno lolote kwa uteuzi huu


Huyu ndiye mkuu mpya wa wilaya ya Iramba mh. LUCY MAYEMBA aliyeteuliwa na J.K.
Sema neno lolote kwa uteuzi huu

Wanasayansi wamegundua kwamba wanaume walio wakarimu na wanaowasikiza wake zao kidole chao cha nne ni kirefu ikilinganishwa na kidole chao cha pili


Wanasayansi wamegundua kwamba wanaume walio wakarimu na wanaowasikiza wake zao kidole chao cha nne ni kirefu ikilinganishwa na kidole chao cha pili.

Je, unakubaliana na utafiti huu uliofanywa na wanasayansi katika chuo kikuu cha McGill University nchini Canada.

Thursday 19 February 2015

FUNDI SAA APOKEA KICHAPO BAADA YA KUDAIWA KUMLAWITI MTOTO HUKO ARUSHA

Njemba mmoja ambaye ni fundi saa maeneo ya Stendi Kuu jijini Arusha leo amepokea kipigo cha mbwa mwizi baada ya kudaiwa kumlawiti mwanafunzi wa kiume wa darasa la tatu wa shule moja jijini humo.

Mapigano ya Magaidi na Polisi Mapango ya Amboni Tanga Hii ndio..........


Mapigano ya Magaidi na Polisi Mapango ya Amboni Tanga Hii ndio Full Story

NI kama kumekucha! Siku chache tu baada ya Gazeti la Ijumaa (ndugu na hili) kuandika ukurasa wake wa mbele habari yenye kichwa; Kiongozi wa kikundi cha kigaidi kinachoua polisi na kuiba silaha kwenye vituo nchini...NI HUYU, kundi jingine limeibuka na kuandika mkanda wa video wakizungumzia uhalifu....


Cha ajabu, sanjari na kundi hilo linalodai liko Tanga, Tanga hukohuko kwenye Kitongoji cha Amboni, Ijumaa iliyopita kulizuka mapigano kati ya polisi, askari wa JWTZ wakipambana na kundi lililodhaniwa ni la kigaidi likiwa limepiga makazi ndani ya mapango ya kihistoria ya  Amboni, Uwazi lina full story.
Katika mapigano hayo hadi juzi Jumapili, askari mmoja wa JWTZ aliuawa huku wanajeshi watatu na askari polisi wawili wakijeruhiwa na kulazwa Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo.

MASHUHUDA WA MAPIGANO 
Kabla Uwazi halijatiririka na video hiyo, lilizungumza na wananchi wenye makazi yao kwenye Kitongoji cha Amboni ambako mapigano ya askari na wahalifu yalitokea.
Mzee Ibrahimu Ally, yeye anasema: “Siku ya tukio (Ijumaa asubuhi) mimi nilikuwa nimepumzika ndani kwangu lakini ghafla nikasikia mlio wa risasi kama mara mbili hivi.

“Mke wangu alikuwa anafua, akaja mbio ndani akisema ni majambazi. Nilimwambia funga mlango haraka sana, akaufunga. Lakini cha ajabu milio ya risasi ikawa inaongezeka kadiri muda ulivyokwenda.
“Ilifika mahali nikajua si majambazi bali tumevamiwa na majeshi ya nje ya nchi. Kwani sasa risasi zilikuwa zikirindima kila muda. Hali ikawa tete kwa kweli. Hata hapa ninapoongea na wewe siamini kama ile milio ya risasi haitajirudia tena.”

WAZIKIMBIA NYUMBA 
Mwanahawa Mudale yeye alisema: “Ilibidi tuhame majumba kwenda kujificha, tatizo ni ile milio ya mabomu na risasi na baadaye tukaona chopa (helikopta) ikitembea angani. Awali tulijua ni vita ya nchi na nchi, kumbe walikuwa askari wetu.”

SIKU MBILI HAKUNA KULALA 
Baadhi ya mashuhuda wanasema kutokana na milio ya risasi kwa siku ya Ijumaa hadi Jumamosi asubuhi, hakuna mwananchi aliyepata usingizi.

“Mimi na familia yangu hatujalala jamani. Risasi na mabomu yasikieni hivihivi tu. Kuna wakati tulikuwa tukiona miale ya moto kutokea kwenye eneo la mapango. Wakati mwingine badala ya moto tuliona moshi mkubwa.
“Kumbe wanajeshi wetu nao walishafika kupambana na hao watu,” alisema Simeon Patrick, mkazi wa Kitongoji cha Karasha, Amboni.

INAVYODAIWA 
Habari zilizosambaa juzi, zinadaiwa kundi hilo lililopambana na askari ni la kigaidi ambapo safari yao kubwa ilikuwa kwenda kufanya ugaidi wa kumwaga damu nchi jirani ya Kenya.

Wale jamaa nasikia walikuwa wakipeleka vifaa nchini Kenya eneo la mwambao ili waje wafanye uhalifu baadaye.
“Sasa wakiwa katika hatua za mwisho mwisho baada ya kupeleka silaha za kivita, wakashtukiwa. Ikabidi waache silala zao eneo walipozificha na wao waje Tanga kujificha kwenye mapango.

“Lengo lao, watulie mpaka hali kule Kenya itakapokuwa imepoa ndipo wajitokeze. Sasa kilichotokea ni kwamba, wakati wanaishi mapangoni ilibidi waanze kutoka kutafuta chakula kwa kufanya uhalifu mdogomdogo ndipo siku moja jamaa yao mmoja akakamatwa kwa uhalifu.

“Yule jamaa ndiye aliyewapeleka polisi walipo wenzake na kutokea kwa mapigano makali kama yale,” alisema mtoa habari mmoja huku akiomba jina lake lihifadhiwe.

WANACHOAMINI WANANCHI, TOFAUTI NA POLISI
Uwazi lilibahatika kuzungumza na baadhi ya wananchi wa jijini Tanga ambapo karibu wote walikuwa na mtazamo mmoja tu.

“Kutuambia wale ni majambazi si sawasawa. Majambazi wetu tunawajua, polisi wanawatosha sana, sasa hawa wametokea wapi mpaka JWTZ washirikishwe?” alihoji Paulina Mathias, mkazi wa Chumbageni, Tanga.

Kusema ukweli serikali ituambie moja. Lakini wale si majambazi. Kwanza mpaka leo hii (juzi) hawajamkamata hata mmoja zaidi ya kujeruhi askari wetu na kumuua mmoja. Wale ni magaidi, lazima tuwe makini sana,” alisema Ally, mkazi wa Duga Maforoni, Tanga.

KUHUSU VIDEO MPYA
Tukiachana na mapigano ya Amboni, sasa turudi kwenye video mpya ya watu waliojiita ni watetezi wa haki dhidi ya udhalimu.
Video hii ipo ndani ya mitandao mbalimbali ya kijamii ambapo wanaonekana watu wawili wakiwa wamevaa mavazi ya kininja ili wasijulikane.




Watu hao wanasema wanapinga jamii yao kukamatwa na kuuawa mara kwa mara wakidai jeshi linawaonea hivyo kutangaza kupambana na askari.
Video hiyo haipishani sana na ile iliyotangulia kuandikwa kwenye gazeti ndugu na hili la Ijumaa.

KAULI YA JESHI LA POLISI
Akizungumza na Uwazi jijini Tanga muda mfupi baada ya kutulia kwa mapambano ya Amboni, Kamishna wa Polisi-Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja aliwataka wananchi kutulia na kuendelea na shughuli zao za kawaida huku akisisitiza:
“Askari walifika mapangoni, kundi lile ni la majambazi. Lilianza kufanya mashambulizi ya risasi na katika majibizano,  askari sita walijeruhiwa na kuwahishwa katika Hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo,” amesema Kamishna Chagonja.    

Thursday 12 February 2015

UN yailaumu Tanzania kwa yanayotokea DRC

Umoja wa mataifa imezituhumu serikali za Tanzania na Burundi kuhusiana na hali katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Ripoti mpya ya kundi la wataalamu wa umoja huo kuhusu Congo, imeituhumu Tanzania kwa kuwaruhusu viongozi wa kundi la waasi wa FDLR kuandaa mikutano nchini humo.
Imeeleza pia kwamba wanajeshi wa Burundi wametekeleza unyanyasaji wa kingono.
Taarifa hiyo ya Umoja wa mataifa inasema kuwa tangu mwaka wa 2013, viongozi wa FDLR na baadhi ya washirika wao wa kisiasa kutoka Ulaya wamekuwa wakikutana nchini Tanzania
Lakini wachunguzi wa Umoja wa mataifa walipoiuliza serikali ya Tanzania kujibu madai haya ilikanusha kabisa kuwahi kuakaribisha mikutano yoyote ya waasi ndani ya ardhi yake na kuongeza kuwa hakujawahi kuwa na mazungumzo yoyote kati ya majeshi yake na wapiganaji wa FDLR.
Umoja wamataifa umesema pia kuwa una ushahidi wa pesa zilizotumwa kutoka taifa hilo la Afrika Mashariki kwa baadhi ya washukiwa nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Ripoti hiyo pia imelaumu kundi hilo la FDLR kwa kutotekeleza ahadi yao ya kusalimisha silaha na kujisalimisha kufikia Januari mwaka huu.
UN inasema kuwa FDLR wamewatuma wazee waliodhoofika kiafya pekee kujisalimisha na kukabidhi silaha chache sana ambazo zina hitilafu.
Kundi la FDLR, liliundwa mwaka wa 2000 na wahutu waliokimbilia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufuatia mauaji ya kimbari ya Rwanda.Kundi hilo linapinga utawala wa kitutsi na ushawishi wake katika eneo la maziwa makuu.
Rwanda imekuwa ikitazama kundi hilo kama tisho kubwa kwa utawala uliopo na kwa kauli moja na Umoja wa mataifa imekuwa ikishinikiza kupokonywa silaha kwa wapiganaji wake.
Ripoti hiyo pia imetoa madai ya ubakaji na unyanyasaji wa kimapenzi unaofanywa na wanajeshi wa Burundi katika Kivu ya Kusini .
Wataalamu hao wa Umoja wa mataifa wamependekeza serikali za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zifanyie uchunguzi madai hayo ambayo wanasisitiza yalifanywa namajeshiya Burundi pamoja na kikundi cha vijana wapiganaji wajulikanao kama Imbonerakure.

zanzibar SAUTI ZA BUSARA......

Alikiba akiwa tayari kwa ajili ya SAUTI ZA BUSARA Zanzibar..... Makamuzi yanaendelea...

Serikali yaiagiza TANESCO kushusha bei ya umeme

Serikali yaiagiza TANESCO kushusha bei ya umeme

Waziri wa Nishati na Madini nchini Tanzania Mh. George Simbachawene amelitaka shirika la umeme nchini (TANESCO) kupunguza bei ya umeme kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia. Soma Zaid hapa
Waziri wa Nishati na Madini nchini Tanzania Mh. George Simbachawene amelitaka shirika la umeme nchini (TANESCO) kupunguza bei ya umeme kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia.
Akizungumza leo jijini Dar es salaam leo mara baada ya kukutana na wafanyabiashara wa mafuta nchini Mh. Simbachawene pia ameishauri mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa
nchi kavu na majini SUMATRA kuona uwezekano wa kupunguza bei za nauli ili wananchi waone faida ya kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia.
Amesema kwa kuwa bei hizo zinapopanda wananchi wamekuwa wakiilalamikia serikali, ni bora pia wakaishukuru serikali kwa kuonja manufaa ya kushuka kwa bei ya nishati hiyo.
Aidha katika hatua nyingine Waziri huyo wa nishati na madini ameitaka mamlaka ya udhibiti wa nishati na maji nchini EWURA kuhakikisha inashirikiana na jeshi la polisi
kudhibiti uchakachuaji wa mafuta ambao kwa sasa umeonekana kufanyika na Ewura pekee bila ya kulishirikisha jesbi la polisi

Saturday 7 February 2015

JE WEST HAM ATAKUFA KWELI KWA KIKOSI HIKI????? TOA MAONI YAKO


HARRY KANE WA SPURS AENDELEA KUWA TISHIO KWA TIMU KUBWA UINGEREZA........ Aipiga Arsenal...

Kane raiya wa England anaendelea kua tishio na kung'aa baada ya kuilaza arsenal kwa mabao mawili,,,,

HIVI NDIVYO ILIVYOKUA INDIA KWENYE SHOW YA DIAMOND

Hii ni moja ya picha ya msanii wa kizazi Kipya Naseeb Abdul marufu kama Diamond alipokua akifanya shoo India jana usiku.. shoo ilikua poa sanaa

Rose Ndauka: Sitazaa Tena Nje ya Ndoa

DIVA wa sinema za Kibongo, Rose Ndauka amefunguka kuwa alikosea kuzaa nje ya ndoa, na sasa hana mpango huo tena.
Rose alisema suala la ujauzito wakati mwingine linaweza kumjia mtu bila kupenda lakini kwa sasa atajitahidi kuona anazaa akiwa ndani ya ndoa.
“Lolote linaweza kutokea lakini kiukweli kwa sasa nitakuwa makini kidogo na ninamuomba Mungu anisaidie mtoto wa pili nimzalie ndani ya ndoa,” alisema Rose ambaye alizaa na Mbongo Fleva, Malick Bandawe kisha kumwagana.
Mwigizaji huyo kwa sasa ameandaa jarida lake ambalo litakuwa linatoka mtaani kila Jumatatu.
GPL

Aunt: Mimba Yangu Siyo ya Waziri!

Muigizaji  wa filamu Aunt Ezekiel Grayson amevunja ukimya na kupinga vikali tetesi za ujauzito wake kuhusishwa na mmoja wa mawaziri wa sasa wa maliasili na utalii  akibainisha kuwa jambo hilo linautesa moyo wake.
Akizungumza na GPL, Aunt alifunguka kwamba, mbali na kumzushia juu ya ujauzito huo, kuwa mara ya kwanza watu asiowajua walieneza uvumi kuwa alikwenda nchini Marekani na mheshimiwa huyo lakini aliwapuuza kwa kuwa alikwenda kwa kazi yake ya sanaa.
“Kuna binadamu hawajali maumivu ya mtu mwingine, inawezekanaje mtu aanze kuropoka kitu kizito kama hicho tena mtu na familia yake, sasa mtu ambaye ndiye muhusika wa ujauzito huu anajisikiaje?
“Ukweli mimba yangu siyo ya waziri, ifahamike kuwa namheshimu sana mheshimiwa, najisikia vibaya mtu anapoeneza kitu cha namna hiyo,” alisema Aunt kwa uchungu mkubwa.
Aunt alitiririka kwamba, mbali na uvumi huo, pia alishangazwa na baadhi ya wabunge waliothubutu kuzungumza kuhusu yeye na waziri huyo tena bungeni kwenye kujadili vitu vya msingi badala yake wanazungumza mambo ambayo hayana kichwa wala miguu.
“Hivi inawezekana kweli kabisa wabunge ambao tunawaheshimu wanakwenda kuzungumza vitu vya ajabu bungeni?
“Wamenifanya nisiwe naangalia hata hilo bunge kabisa,” alisema Aunt.
Staa huyo alimalizia kuwa mambo hayo yanampa wakati mgumu na kumuumiza kwa sababu madai yanayozungumzwa ni mazito huku yakiwa hayana chembe ya ukweli zaidi ya kuleta mfarakano kwenye familia ya waziri huyo ambaye pia ni mbunge.
Mbali na waziri huyo, pia Aunt alikanusha kuwa mimba kubwa aliyonayo si ya yule mcheza shoo wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, Mose Iyobo kama wengi wanavyodai.
Kuhusu hilo, GPL lilizungumza na Mose Iyobo ambaye alisema kuwa anachojua ujauzito ni wa kwake lakini akashangazwa na uzushi usiokuwa na kichwa wala miguu.
Swali ni je , kama Aunt anamruka Mose Iyobo na amekasirishwa na tetesi za kuhusishwa na waziri huyo ambaye ni mume wa mtu huku mumewe, Sunday Demonte akidaiwa kufungwa Dubai, je, mimba hiyo ni ya nani?

Friday 6 February 2015

[ Zari Hassan kufunga ndoa na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, "Asema hakuna umri maalumu wa Kuoa au Kuolewa

WAKATI mama mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kasim ‘Sandra’ akiwa nchini India kwa matibabu ya tatizo la kiafya linalodaiwa kuwa ni kupooza, hapa Bongo dalili za Diamond na mpenzi wa

Friday 30 January 2015

NIPIGE MKE WANGU MAANA MDA MWINGINE NAKOSA ADABU!!


Friday, January 30, 2015

Shilole aomba radhi kwa kumdunda Nuh Mziwanda .......Nuh naye kasema yupo tayari kupigwa mpaka AKOME!!!


Baada ya Shilole  kumchapa vibao mchumba wake Nuh Mziwanda, Shilole amelazimika kuomba radhi.

Shilole amewaomba radhi mashabiki wake kwenye mtandao wa Instagram kwa kupost picha akiwa na mpenzi wake huyo na kuandika:

 

“Huyu hapa mjanja wangu mimi, daah nimekamatika hapa, na naamini ni mwanaume sahihi kwangu maana hawezagi kurusha hata ngumi japo namchokozaga mie mjeuri tu, mnao muhandama mme wangu mmeshindwa, kugombana ni kawaida sana kwenye mapenzi na kama nliwaudhi mashabiki wangu mnisamehe mie nampenda mme wangu.”

 

Naye Nuh Mziwanda aliandika:

Mwanaume lijali aliekamilika ampigi mpenzi wake wala kurudishia kibao au kofi alilopigwa na mpenzi wake.naamini kwenye mapenzi ya kweli wivu lazima na kugombana kwenye mapenzi ni kama kwenda chooni ni swala la kawaida sana.aaaaaaaya mke wangu nimekup rukhsa nipige mpaka nikome.ila all i know its love dats it.Nawapenda Mashabiki wangu pamoja sana .#zimaTaa sie tayari

Tuesday 27 January 2015

Ushuhuda Huu wa Mzungu Kuhusu Wauza Madawa ya Kulevya

Jan 26, 2015

Ushuhuda Huu wa Mzungu Kuhusu Wauza Madawa ya Kulevya 'Unga’ Ufanyiwe Kazi

Kwa zaidi ya wiki tatu sasa, Watanzania wamekuwa wenyeji wa mgeni ambaye ujio wake nchini umekuwa wa aina yake. Tunaweza kusema ugeni huo siyo wa kawaida, kwani tumezoea kuona ziara za wanasiasa, wafanyabiashara na wageni wengine wengi kutoka katika mataifa mbalimbali wanaokuja kwa ziara za kiserikali na nyinginezo, mbali na watalii wanaotembelea nchi yetu kujionea vivutio lukuki vilivyosambaa kila sehemu.

Hata hivyo, ziara ya Padri John Wootherspoon, raia wa Australia aliyekuja nchini Januari Mosi, mwaka huu ni tofauti kabisa na ziara nyingine tulizozizoea. Yeye anaishi China na amepata kibali cha Serikali ya China kutembelea magereza mbalimbali nchini humo na kuwafariji wafungwa. Katika kufanya kazi yake hiyo katika magereza nchini China na majimbo yake ya Hong Kong na Macau, amekutana na wafungwa wengi kutoka nchi mbalimbali duniani na kugundua kwamba kilichowaingiza magerezani ni biashara ya dawa za kulevya.

Kabla ya kuja hapa nchini, Padri Wootherspoon aliliambia gazeti hili, ambalo kwa muda mrefu limekuwa likifuatilia huduma zake katika magereza nchini China kuwa, alikuwa na mpango wa kuitembelea Tanzania baada ya kugundua kwamba idadi ya Watanzania wanaotumikia vifungo katika magereza mbalimbali nchini China ni kubwa mno ikilinganishwa na wafungwa wengine kutoka nchi nyingine. Anasema wafungwa zaidi ya 130 kutoka Tanzania wako katika magereza ya Shek Pik, Stanley, Loo Woo na Macau na kwamba kila mwezi Watanzania wanne hadi sita wanafungwa magerezani kwa makosa hayo.

Kutokana na hali hiyo, Padri Wootherspoon aliamua kuja Tanzania kwa gharama zake mwenyewe ili kuwasaidia wafungwa hao kuwasiliana na familia zao hapa nchini, baada ya kupata mawasiliano ya familia hizo kutoka kwa wafungwa hao. Anasema wafungwa hao walitumiwa tu na wafanyabiashara wakubwa (ambao majina yao tunayahifadhi kwa sasa) kupeleka dawa hizo nchini China na kwamba tangu awasili nchini amewasiliana na familia nyingi za wafungwa hao, ambazo amesema zimo katika umaskini mkubwa. Padri huyo tayari amekutana na Kamishna wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya, ACP Godfrey Nzowa na kumtaka aende nchini China kupata taarifa za kina kutoka kwa wafungwa hao.

Sisi tunadhani ziara ya Padri huyo hapa nchini ni fursa ya pekee kwa Serikali kupata taarifa muhimu za kusaidia kutokomeza biashara hiyo. Juni, mwaka jana Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi alisema wakati wa kuadhimisha Siku ya Kupiga Vita Matumizi na Biashara ya Dawa za Kulevya Duniani kwamba kazi ya kuwanasa vinara wa biashara hiyo imekuwa ngumu na akisema vijana wa Kitanzania 65 kati ya 403 waliokamatwa nchi za nje kwa kuhusika na usafirishaji wa dawa za kulevya wamehukumiwa kunyongwa nchini China.

Waziri Lukuvi pia alisema vitendo vya rushwa vimekwamisha jitihada na mikakati ya kuwatia mbaroni vigogo wa biashara hiyo. Bahati nzuri ni kwamba Padri Wootherspoon yuko nchini kama sehemu ya suluhisho la tatizo hilo.

Ni matarajio yetu kwamba Serikali itafanya kila linalowezekana kushirikiana naye ili kupata taarifa muhimu zitakazosaidia kuwakamata wamiliki wa biashara hiyo. Hatua hiyo pia itaondoa dhana iliyojengeka miongoni mwa wananchi kwamba kikwazo kikuu katika vita ya kukomesha uhalifu huo kimo ndani ya Serikali yenyewe.

Mama wa Mapacha sita anunuliwa nyumba

Tuesday, 27 January 2015

Mama wa Mapacha sita anunuliwa nyumba

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Covenant Bank Balozi, Salome Sijaona(Katikati) akikata utepe, kuashilia uzinduzi Rasmi wa nyumba aliyokabidhiwa Salome Mhando ambaye alitelekezwa na mume wake baada ya kujifungua watoto mapacha mfurulizo hadi kufikia sita na kukosa Mahali pa kuishi, Covenant Bank imemkabidhi nyumba hiyo ambayo ataimiliki yeye mwenyewe pamoja na thamani za ndani na Bima ya Matibabu kwa Mwaka mzima. Anaeshuhudia ni mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Sabetha Mwambenja (wa kwanza kushoto) na Salome Mhando (wa kwanza kulia).

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Covenant Bank Balozi, Salome Sijaona (kushoto), Pamoja na Mkurugenzi wa benki Hiyo, Sabetha Mwambenja, wakimkabidhi hati ya kiwanja na Umiliki wa nyumba Salome Mhando, Mama alietelekezwa na mume wake baada ya kujifungua watoto mapacha mfurulizo, hadi kufikia sita, Benki hiyo imemkabidhi nyumba hiyo pamoja na Bima ya Matibabu kwa mwaka mzima

AIBU ILIOJE


Tuesday, January 27, 2015

AIBU: Shilole Amchapa Makofi Mpenzi wake Nuhu Mziwanda


Jumamosi iliyopita ndani ya Tamasha la Kiboko Yao lililofanyika Leaders Club, Gazeti la Makorokocho lilishudia live Msanii Shilole akimchezeshea kichapo mchumba wake Nuh Mziwanda kwa madai kuwa Nuh alikua hataki kuondoka nae eneo la tukio....

 

Mchekeshaji Steve Nyerere alijitokeza kuamulia ugomvi na kufanikiwa kumtoa Shilole eneo lile lakini baada ya muda Shilole akarudi na kumdai funguo ya gari Nuh ambaye siku hiyo alionekana kuwa mpole ikabidi mabaunsa waingilie kati na kumtoa kwa nguvu shilole....

 

Baadae Nuh alionekana akitoa machozi na Malkia wa Taarabu Khadija Kopa alionekana akimbembeleza na kumfuta machozi.

Monday 26 January 2015

Mwanamke Awaua watoto wake wawili na Kuwazika ndani ya Nyumba Yake

Mwanamke Awaua watoto wake wawili na Kuwazika ndani ya Nyumba Yake


Mwanamke mmoja  mkazi wa mkoa wa Tabora wilaya ya Tabora mjini kata ya Chemchem amewaua watoto wake wawili  na kuwazika ndani ya nyumba yake.

Mwanamke  huyo  amedai  kuwa  kilichomfanya  awalishe  sumu  watoto  wake  ni ugumu  wa  maisha  uliokuwa  ukimkabili  baada  ya  kikimbiwa  na  mumewe. 


Kwa  mujibu  wa  jirani  yake, siku  ya  tukio  mwanamke  huyo  alisikika  akichimba  shimbo  ndani  ya  nyumba  yake  kabla  ya  kutangaza  kupotelewa  na  watoto  wake  siku  ya  pili  yake.

Taarifa  ya  kupotea  kwa  watoto  hao   ilimpa  mashaka  jirani  huyo  na  kumlazimu  akatoe  taarifa  polisi  ambapo  maafande  walikuja  na  kufanya  msako  ndani  ya  nyumba  hiyo  ambapo  walifanikiwa  kufukua  maiti  za  watoto  hao. 

Saturday 24 January 2015

TUKIO LA KINYAMA:MWENYEKITI AKATWA KICHWA NA SEHEMU ZA SIRI KISHA KUWEKWA KWENYE SUFURIA

Ni Tukio la kuskitisha sana ktk kijiji cha songambele wilayan MLELE mkoan KATAVI watu wasiofahamika wamemvamia mwenyekiti wa kijiji cha songambele na kisha kutenganisha kichwa na kiwiliwili na pia sehemu zake za siri na kisha kukata mkono wake mara mbili baada ya kufanya kitendo hicho walichukua viungo walivyokata kutoka kwa mwenyekiti huyo na kisha kuvitia kwenye sifuria wakaweka maji na kisha kubandika kwny moto n kuanza kuvipika baada ya Tukio Hilo watu hao walitokomea sehemu isiyofahamika polisi wilayan MLELE wanaendelelea n uchunguz kubaini wahusika wa tukio Hilo. Tukio Hilo limetokea leo majira ya saa saba ucku hayo ndo yaliyojir wilayan kwetu MLELE

KATI YA ZARI 41, NA WEMA 26.... YUPI BORA..................................... DIAMOND NDO MWENYE MAJIB

The younger Wema Sepetu:And then the old Zari                                                                                                                                                                                                        And please not that this lady is 41 years old!
What is it about older women? I have heard it said that the key weapon in an older woman’s arsenal is that she knows how to treat a man but my response is always that a man is not a cat! A man is not feline to be kept. Men are hunters.
Then there is the usual almost cliche rebuttal that a young girl while sweet is usually a bucketload of drama. What do you think?                                                                                                                                                                                                                                                                      If you were to ask Diamond, he would probably say that older ladies are sweeter. Something to do with fine wine and time but what do I know? Personally, I am one of those who believe that raw mangoes taste infinitely better because you can add pilipili and salt to them. Perhaps you like my friend Chege Miati prefer old squishy mangoes. I do not know.
But you see, Diamond dated Wema Sepetu, a young -er lass for quite some time. Sadly, that union ended when he decided to dump her the same way we through day old cold porridge outside the window the very moment he saw Zari, the 41 year old MILF.
Compare the two if you would

MATOKEO KOMBE LA FA MPAKA SASA......

Matokeo ya michuano ya FA jumamosi kufiki sasa
Blackburn 3 - 1 Swansea FT
Birmingham 0 - 2 West Brom L
Cardiff 1 - 0 Reading L
Chelsea 2 - 1 Bradford L
Derby 1 - 0 Chesterfield L
Man City 0 - 0 Middlesbrough L
Preston 1 - 0 Sheff Utd L
Southampton 2 - 3 Crystal Palace L
Sunderland 0 - 0 Fulham L
Tottenham 1 - 0 Leicester L

Rais Kikwete awateua mawaziri 8 Tanzania

Rais Jakaya kikwetu wa Tanzania ametangaza mabadiliko katika baraza lake la mawaziri.
Rais amewateua mawaziri wanane wapya pamoja na manaibu watano.
Tangazo hilo lilifanywa na katibu katika ikulu ya rais balozi Ombeni Sefue.
Mabadiliko hayo yanajumuisha wadhfa wa waziri wa nishati na kawi wa Profesa Muhongo ambaye amejiuzulu mapema leo pamoja na wadhfa wa waziri wa ardhi ambao uliwachwa wazi baada ya kupigwa kalamu kwa Anna Tibaijuka.
Mawaziri hao wawili wanahusishwa na kashfa ya ufisadi ambayo ilimshinikiza mwanasheria mkuu pia kujiuzulu.
Rais Kikwete anatarajiwa kuwaapisha mawaziri hao wapya hii leo katika tangazo litakalorushwa hewani na runinga ya taifa

MAMBO YA KUZINGATIA UKIWA NA UJAUZITO

Ujauzito ni safari ndefu inayomchukua mwanamke miezi tisa au majuma arobaini hadi kujifungua. Ni safari yenye mikikimikiki na hatari nyingi kwa mama na mtoto. Tusichukulie suala la ujauzito kama jambo la kawaida ingawa pia ni wajibu kwa mwanamke.

Ujauzito siyo hali ya hatari au kutisha endapo mambo ya msingi yatazingatiwa kabla ya kuwa mjamzito na kipindi cha ujauzito hadi baada kujifungua. Katika kipindi cha ujauzito kuna mambo mengi ambayo ni mabadiliko humtokea mama na mtoto aliye tumboni.
Katika makala haya tutazungumzia mambo ya kuzingatia kabla ya kuamua kubeba mimba, siyo kila mwanamke anaweza kubeba mimba kwa sababu wengine huwa na matatizo katika mfumo wao wa uzazi, aidha homoni zao hazifanyi kazi vizuri na mayai hayazalishwi au hayapevuki.
Huenda pia mirija ya uzazi imeziba au ana matatizo ndani ya kizazi.

NINI CHA KUFANYA?
Ni vyema upange sasa unataka kuwa mjamzito au mwezi fulani unataka kushika mimba, uwe na mpango. Hata hivyo, hakikisha umri wako upo zaidi ya miaka 20 kwa usalama zaidi wa afya yako.
Mshirikishe mwenzi wako na mwambie ungependa upate ujauzito, siyo vizuri kushtukiza kwani inaweza kukupa ‘stress’ wewe mwenyewe au mwenzako endapo mmoja wenu hajajiandaa kisaikolojia.

CHEKI AFYA YAKO
Hakikisha una afya njema, huna magonjwa sugu kama kisukari, shinikizo la damu, magonjwa mengine ya moyo, kansa, HIV, kifafa, pumu, siko seli au grupu lako la damu ni RH negative.Endapo una matatizo haya hapo juu, basi haraka wasiliana na daktari wako wa masuala ya uzazi akupe ushauri kwani magonjwa mengine yatakusumbua wakati wa ujauzito, au magonjwa yenyewe yatamwathiri mtoto.

Hakikisha huna magonjwa au matatizo katika viungo vya uzazi, mfano kutokwa na uchafu ukeni wenye muwasho na harufu mbaya, vipele au vidonda sehemu za siri, maumivu wakati wa tendo la ndoa, kutokwa na damu au usaha ukeni. Vile vile mfumo wako wa uzazi uwe vizuri, matatizo katika mfumo wa uzazi ni kama vile maumivu ya tumbo chini ya kitovu, kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi, kutopevusha mayai na kukosa hamu ya tendo la ndoa.
VILEVI ACHA
Epuka unywaji wa pombe na uvutaji wa sigara, hili hata kwa mwanaume anayetaka mtoto.
Mwanamke kabla ya kuwa mjamzito hakikisha unakula sana mboga za majani ili upate kiwango kizuri cha vitamin ya Folic Acid, ni vema ule sana mboga za majani au upate virutubisho vya Folic Acid. Endapo hutakuwa na kiwango kizuri cha Folic Acid, kuna hatari ya kuzaa watoto wenye matatizo.

MAZOEZI
Fanya mazoezi mepesi mara kwa mara ili kuimarisha nyonga na viungo vyako vingine na usipate matatizo wakati wa kujifungua. Pata ushauri wa daktari kipindi muafaka.

YANAYOKWAMISHA UJAUZITO
Matatizo yanayoweza kukusababishia usipate mimba ni kutofahamu siku za kupata mimba, kuziba mirija ya uzazi.Pia uwepo wa uvimbe ndani ya kizazi na kwenye vifuko vya mayai. Uvimbe wa aina hii unaweza kutibika kwa dawa na ukaisha au kwa njia ya upasuaji, inategemea na daktari wako atakavyoona na kuamua.

Kwa upande wa wanaume wanaojiandaa kuwa wazazi, ni vema umjulishe mpenzi wako sasa unataka mtoto au lini unataka mtoto. Tibu magonjwa yanayoathiri mfumo wa uzazi, mfano maumivu ya korodani, maumivu ya njia ya mkojo, upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume. Kutoa manii mepesi sana kiasi kwamba baada ya tendo la ndoa manii zote zinatoka ukeni.
Ni vema ukapime mbegu zako za kiume kuona kama zina ubora wa kutosha, usiwe na maumivu yoyote ya mwili kwani yataweza kukusababishia kupunguza nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa.

Nigeria (nollywood) nao wafanya madudu kama bongo movies.......

            whats Wrong With This Photo from Nigerian Movies?! wavaa nguo za ajabu ambazo ziko nje ya maadili..... af zaidi ukiangalia kwa nyuma kuna kioo ambacho kinaonesha wapiga picha na watu wengine ambao sio sehemu ya kipande hichi cha movie

TIKO AWAVAA WANAUME!!!


Saturday, January 24, 2015

Tiko Awavaa Wanaume Wanaodai yeye ni GOGO Kitandani


Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Tiko Hassan amesema hakuna kauli ambayo haipendi kama kuambiwa si hodari wa mapenzi (gogo) wakati anajiamini yupo vizuri katika sekta hiyo.

Tiko alifunguka kauli hiyo alipokuwa akifanya mahojiano na mwandishi wetu na lilipofika suala la malovee, Tiko aling’aka vibaya mara baada ya kuambiwa kuwa kuna marafiki zake wanamuita gogo.

 

“Wee nani kasema? Sipendi kuitwa hivyo wakati mwenyewe najijua kabisa ninakuwaje pindi ninapokuwa na mpenzi wangu, najiamini kweli,” alisema Tiko

Majambazi Yaitikisa Zanzibar


Saturday, January 24, 2015

Majambazi Yaitikisa Zanzibar


Jeshi la polisi Zanzibar kwa kushirikiana na wafanyabiashara wa machinga walioko darajani Zanzibar  wamefankiwa kuwakamata majambazi wawili  huku kukiwa na taarifa kuwa mmoja amefariki baada ya kutupiana risasi  na kusababisha kizaazaa cha aina yake mjini Zanzibar.

 

Hali hiyo imetokea baada ya  polisi  kuanza  kuwasaka na kuyafuata majambazi hayo ambayo baada ya kuona wamenaswa  wakaamua kukimbia na kuingia maeneo ambayo yanatumiwa na wafanyabishara  wadogo wadogo maarufu kwa jina la  'dada njoo'.

  

Baada ya kuingia katika maeneo hayo, ndipo wafanyabishara hao wakaanza kuwanasa nakuwabana majambazi hao yaliokuwa katika gari aina ya Noah yenye namba  za usajili ambazo inasemekana ni za bandia.

 

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mjini Magharibi Muccadam Khamis amesema polisi bado inawasaka wengine ingawa amesema uchunguzi unaendelea  na kuthibitisha kuwepo kwa wananchi wanane ambao walipatwa mshtuko na wako hopitali ya Mnazi Mmoja  wakipata  huduma za matibabu.

  

Hata hivyo taarifa zilizopatikana mjini Zanzibar zinadai kuwa jambazi moja ambaye anajulikana kwa jina la Khmais Mabunduki na ambaye alikuwa anasakwa na polisi kwa muda mrefu ndiye aliyefariki kutokana na mapigano hayo, huku bado polisi wakiendelea kuwasaka wengine ambao wako katika mtandao mmoja.